logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho:Jamaa aachwa baada ya kurudi nyumbani akiwa mlevi na kuangukia mboga alizopika mkewe

Jose alieleza kwamba mkewe alikasirika kufuatia vurugu za kinyumbani zilizotokea wakati alirudi akiwa mlevi.

image
na Samuel Mainajournalist

Patanisho03 April 2025 - 09:13

Muhtasari


  • Jose alisema ndoa yake ya mwaka mmoja unusu ilisambaratika Desemba mwaka jana wakati mkewe alitoroka na kurudi nyumbani kwao.
  • "Alichelewa kufungua mlango nikausukuma nikaanguka huko kwa mboga. Akaanza kuniambia ‘Sasa tutakula nini?’" Jose alisema.

Ghost na Gidi

Jamaa aliyejitambulisha kama Jose Indeche (28) kutoka Mumias alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mke wake Sharon Iminza (24) ambaye alikosana naye miezi kadhaa iliyopita.

Jose alisema ndoa yake ya mwaka mmoja unusu ilisambaratika Desemba mwaka jana wakati mkewe alitoroka na kurudi nyumbani kwao.

Alieleza kwamba mkewe alikasirika kufuatia vurugu za kinyumbani zilizotokea wakati alirudi akiwa mlevi.

“Ilikuwa Desemba 2023 tukaenda sherehe ya vijana kunywa pombe kiasi. Nilirudi nyumbani usiku kama nimelewa, sikuwa najielewa nikaanguka kwa mboga yenye alikuwa amepika hapo. Alichelewa kufungua mlango nikausukuma nikaanguka huko kwa mboga. Akaanza kuniambia ‘Sasa tutakula nini?’. Nikamwambia anyamaze ati ni yeye hakuwa ameweka mboga vizuri. Akanipiga kofi. Nilihuzunika sana,” Jose alieleza.

“Nikijaribu kumpigia, sijui aliweka simu yangu block. Sikuwa nimeenda kwao bado, ndio maana nimewapea namba ya baba mkwe. Nikipiga baba mkwe anakuwa mkali. Nilikuwa nimeishi na huyo msichana kwa mwaka mmoja unusu. Nilikuwa nataka niongee na Sharon nimuombe msamaha kama nimekosea turudiane na yeye. Ningetaka turudiane tuweze kusaidiana,” aliongeza.

Kwa kuwa Jose alituma namba ya baba mkwe, alipigiwa simu na kufichua kwamba alikerwa na jinsi kijana huyo alimpiga bintiye.

“Huyo msichana bado hajamuoa rasmi. Mambo ya msichana siwezi jua vizuri lakini kuna kitu huyo jamaa alimfanyia sikufurahia. Alirudi usiku na akampiga. Vile alimpiga sikufurahia,” Babake Sharon alisema.

Jose alichukua fursa hiyo kuomba msamaha akidai kwamba bado anampenda sana.

“Najua niliwakosea lakini ningependa mnisamehe. Bado napenda huyo msichana. Tulibishana naye lakini nitakuja tuongee kabisa. Nitatafuta nafasi. Lazima nitafute kitu ndio nikuje huko,” alimwambia baba mkwe.

“Msichana alikuwa anasema wazazi walikufa. Hakuwa anataka nijue kwao. Alitaka nimalize kujenga kwanza,” aliongeza.

Babake Sharon alimwambia, “Utakuja vipi? wakati ukikuja unabaki kwa gate huko.  Kutoka uchukue msichana wangu. Umewahi kuja kwangu. Hiyo mwaka moja na nusu, hukuwa unajua njia ya kuja kwangu? Wewe jipange ukuje tuongee.”



RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved