logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Patanisho: Jamaa amfungia mkewe nje usiku baada yake kukosa kumpikia chakula cha jioni

Ayub alighadhabika baada ya kuamka na kupata  chakula bado hakijawa tayari.

image
na Radio Jambo

Habari04 May 2022 - 05:25

Muhtasari


•Jane alisema mumewe alighadhabika sana baada ya kuamka na kupata  chakula bado hakijawa tayari. 

•Ayub alisita kumsamehe Jane huku akisisitiza kuwa ni sharti aende nyumbani kwake ili kwanza washiriki mazungumzo ya moja kwa moja.

Ghost na Gidi

Jane Esokoma ,25, alituma ujumbe alituma ujumbe akiomba kupatanishwa na mume wake Ayub Simiyu ambaye walikosana naye kufuatia ugomvi wa kinyumbani.

Mama huyo wa mtoto mmoja alisema ndoa yao ya miaka mitano ilisambaratika mwezi Julai mwaka jana baada ya mumewe kurejea nyumbani na kupata bado hajapika.

"Nilifika nikiwa nimechelewa. Nilikuwa nabomoa nywele. Alifika kwa nyumba akaanza kugombana nami. Aliniuliza mbona sipiki nikamwambia bado ni mapema. Niliendelea kubomoa nywele akaenda kulala. Baada ya muda aliamka akanipata bado nabomoa nywele," Jane alisimulia.

Jane alisema mumewe alighadhabika sana baada ya kuamka na kupata  chakula bado hakijawa tayari. 

Kuona hivyo mwanadada huyo aliamka na kuenda jikoni kuandaa chakula ila mumewe akamfuata na kuzima moto ule kutumia maji.

"Nilitoka nje nikaenda jikoni akaja akamwaga maji kwa moto. Niliwasha moto tena akaja akamwaga maji tena. Nikawasha mara ya tatu akafanya vilevile. Alinifungia nje mpaka saa tisa usiku," Alisema.

Ayub alipopigiwa simu alisita kumsamehe Jane huku akisisitiza kuwa ni sharti aende nyumbani kwake ili kwanza washiriki mazungumzo ya moja kwa moja.

Alitilia shaka ahadi ya mkewe kuwa angeepiga hatua ya kurudi huku akifichua kuwa amewahi kuahidi tena kurudi ila hakurudi.

"Unasema hivo hapo lakini najua hutakuja. Kama unataka msamaha njoo uniombee nyumbani sio hapo kwa redio. Amesema mara mingi atakuja alafu hakuji," Ayub alisema.

Ayub alimsihi mkewe arudi ili waendelee kulea mtoto wao pamoja. Jane alimhakikishia Ayub kuwa bado anampenda na kumuahidi kuwa angerudi ili waweze kuendelea kuishi pamoja..


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved