logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mpenzi wangu anajua nafanya kazi kwa 'supermarket' lakini nafanya kwa chumba cha kuhifadhi maiti-Mwanamume atoboa siri

Pia kuna watu ambao wanakataa kazi fulani kwa ajili ya wapenzi wao.

image
na Radio Jambo

Michezo25 January 2021 - 22:04

Muhtasari


  • Mwanamume aeleza kazi anayofanya kinyume ya yale mpenzi wake anajua
  • Mwanamume huyo alifichua kwamba anafanya kazi katika chumba cha kuhifadhi maiti lakini mpenzi wake anajua anafanya kazi kwa supermarket 

Katika kipindi cha toboa siri kwenye radiojambo, siku ya Jumatatu mwanamume mmoja aliwashangaza wengi baada ya ufichua kazi ambayo anafanya kinyume ya yale mpenzi wake anajua.

Kwa kweli lazima kila mtu afanye juu chini ili apate riziki ya kila siku na kuweka chakula mezani mwake.

Lakini kuna baadhi ya watu ambao hawawezi kufanya kazi fulani kwa maana wamesoma na wamehitimu na shahada kuto kwenye chuo kikuu.

Pia kuna watu ambao wanakataa kazi fulani kwa ajili ya wapenzi wao.

Huu hapa usimulizi wake;

"Ninafanya kazi katika chumba cha kuhifadhi maiti, lakini mpenzi wangu anajua kwamba nafafanya kazi kwa duka kubwa yaani supermarket

nimeamua kutoboa siri kwa maana anakuja mwezi ujao kuishi na mimi, huwa nafanya kazi yangu usiku alafu natoka mchana

Huwa naosha maiti, nataka ajue kutoka leo kwa maana nampenda sana, sijui kama ataniacha baada ya kusikia haya au atazidi kunipenda." Alieleza Mwanamume huyo.

Je mpenzi wako anafahamu unafanya kazi gani, na unaweza kuacha kufanya kazi kwa ajili mpenzi wako hapendi kazi hiyo?

 

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved