logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nilipeleka 'boxer' yangu kwa mganga ili nisiwahi kosa kazi-Mwanamume amtobolea mkewe siri

Huku akisimulia jinsi alipeleka 'boxer' yake kwa mganga ili apate kazi alisema kwamba huvaa, 'boxer' hiyo kila siku.

image
na Radio Jambo

Habari22 March 2021 - 15:01

Muhtasari


  • Mwanamume atoboa siri jinsi alipeleka 'Boxer' kwa mganga

Katika kipindi cha mbusi na lion teketeke, mwanamume mmoja alimtobolea mkewe siri kuhusu 'boxer' yake na jinsi huwa anapata kazi.

Huku akisimulia jinsi alipeleka 'boxer' yake kwa mganga ili apate kazi alisema kwamba huvaa, 'boxer' hiyo kila siku.

"Nilipeleka boxer yangu kwa mganga ili nikuwe nikipata kazi kila siku, kwa maana mimi ni mtu wa kibarua

Kuna wakati mke wangu alificha boxer hiyo na nilikuwa nikienda kutafuta kazi naambiwa hamna kazi kwa wiki nzima

Nataka kumtobolea siri kwamba boxer hiyo ambayo huwa nafua na navaa kesho yake ndio hutafuta unga wa kila siku

Mganga aliniambia ikizeeka naeza nunu ingine nimplekee, akaniwekee dawa tena, sasa nimeivalia kwa miaka miwili," Alisimulia mwanamume huyo.

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved