logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Mganga alinipa kifaranga mtu ambaye nimekuwa nikifanya tendo la ndoa naye-Mwanamume amwaya mtama

Kulingana na mwanamume huyo usiku ukifika kifaranga huyo amekuwa akibadilika na kuwa mwanamke.

image
na Radio Jambo

Habari07 July 2021 - 15:17

Muhtasari


  • Katika kitengo cha toboa siri jamaa mmoja alwaacha mashabiki wa radiojambo na mshtuko baada ya kutoboa yale amekuwa akifanya baada ya kupewa kifaranga na mganga
  • Kulingana na mwanamume huyo usiku ukifika kifaranga huyo amekuwa akibadilika na kuwa mwanamke

Katika kitengo cha toboa siri jamaa mmoja alwaacha mashabiki wa radiojambo na mshtuko baada ya kutoboa yale amekuwa akifanya baada ya kupewa kifaranga na mganga.

Kulingana na mwanamume huyo usiku ukifika kifaranga huyo amekuwa akibadilika na kuwa mwanamke.

Lakini kwanini alienda kwa mganga na kupewa kifaranga huyo?

"Kuna msichana ambaye alikuwa ananikataa sana na nilikuwa nampenda sana, nilienda kwa mganga ili anitengenezee mambo ili anipende

Alinipa kifaranga kwa shilingi elfu nne, na kuniambia napaswa kumpa chakula na maji, na kunihakikishia mambo yangu yatkuwa sawa

La kushangaza ni kuwa usiku ukifika kifaranga huyo amekuwa akibadilika na kuwa mwanamke, nimekuwa nikifanya tendo la ndoa naye kwa muda wa wiki moja

Nataka kumtobolea mpenzi wangu kwamba nina jini mwanamke ambaye amekuwa nami, ndio maana sina hisia zake," Alieleza jamaa huyo.

Jamaa huyo alitaka kumtobolea mpenzi wake siri hiyo, na je ingekuwa ni wewe au ingekuwa ni mpenzi wako ungefanya nini baada yake kukutobolea siri kama hiyo.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved