logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Nimemwajiri mpango wangu wa kando kama kijakazi wangu-Jamaa atoboa siri

Katika kitengo cha toboa siri, jamaa ameeleza jinsi amemwajiri mpango wake wa kando kama kijakazi wake.

image
na Radio Jambo

Burudani12 October 2021 - 15:00

Muhtasari


  • Katika kitengo cha toboa siri, jamaa ameeleza jinsi amemwajiri mpango wake wa kando kama kijakazi wake

Wakishindwa kuziweka huwa wanamwaya mtama katika kitengo cha toboa siri, je unamfahamu mke wako au mume wako vyema?

Karne hii ya sasa asilimia kubwa ya wanandoa hawatambui tamaduni za ndoa, kwani wamekuwa wakitafuta mipango ya kando ili kutimiza mahitaji yao.

Katika kitengo cha toboa siri, jamaa ameeleza jinsi amemwajiri mpango wake wa kando kama kijakazi wake.

Kulingana na mwanamume huyo, mkewe alimpa ruhusa ya kutafuta kijakazi kutoka kwao, na kumwendea mpango wake wa kando.

"Nimekuwa kwa ndoa kwa miaka 7, nimekuwa nikiajiri wafanyakazi na mke wangu anawafukuza kila mwaka

Aliniambia niende nikalete kijakazi kutoka kwetu nyumbani, nilienda na kumleta mpango wangu wa kando awe kijakazi wetu

Mke wangu hajui kama huyo ni mpango wangu wa kando, nataka kumtobolea siri nimwambie kwamba kijakazi huyo ni mpango wangu wa kando, kwa hivyo ajue ana mke mwenza

Nimetoboa siri hii, kwa sababu mpango wa kando alinitishia atamwambia mke wangu ukweli," Alisimulia

Je ni ushauri upi unawea mpa mwanamume huyu?

 

 

 

 

 


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved