

Kutoka kwenye fukwe zilizokuwa zimesahaulika za Coco Beach katika jiji la pwani la Dar es Salaam, Tanzania, shirika la kiraia la ndani linaongoza wimbi ya ajabu la urejeshaji wa mazingira.
Kwa kuchanganya uhufadhi endelevu na uwezeshaji wa kijamii, Africraft inageuza pwani chafu kuwa mali ya jamii inayostawi na kuchochea harakati kubwa ya kitaifa.
"Tunawageuza wakusanyaji taka wa mitaani kuwa wabadilishaji taka rasmi," anasema Robertho Vasco Njovu, Mratibu wa Mradi wa Usimamizi wa Taka wa Africraft.

Mara mbili kwa wiki — Jumatatu na Ijumaa — timu ya vijana 10 hulinda kipande cha kilomita tatu cha Coco Beach, wakikusanya hadi kilo 400 za taka.
Wakiwa wameacha kazi za zamani za kukusanya taka mitaani, sasa wanavaa vifaa vya kujikinga binafsi na hufanya ukaguzi wa chapa ili kusaidia uhifadhi wa bahari na kuongeza uelewa wa umma.
Njovu alizungumza na Xinhua kutoa Kituo cha Taarifa na Usimamizi wa Taka (WIM), jengo lililotengenezwa kwa nyasi za ufumaji (raffia), majani ya minazi, vifuniko vya chupa na vioo.
"Kituo cha WIM ndicho kituo chetucha amri, kitovu chetu na darasa letu," alieleza Njovu.
"Kinatukumbusha kila siku kwamba jamii zikijali, mazingira hupona."
Aina kuu za taka zinazokusanywa ni pamoja na chupa na vifungashio vya plastiki kutoka maji, juisi na vinywaji vya kuongeza nguvu, pamoja na chupa za kioo kutoka bia, divai na vileo kama vile gin.
Vipande vidogo vya plastiki kama vile vifuniko vya chupa, mirija ya kunywea, na vifungashio vya barafu pia hupatikana kwa wingi.
"Vifaa vinavyoweza kutumika husafirishwa hadi makao makuu yetu kwa ajili ya kubadilishwa. Vitu ambavyo hatuwezi kutumia tena hupelekwa kwa wanachama wa Chama cha Wachakataji Taka Tanzania, ambacho kina zaidi ya wachakataji 100," alisema Njovu.

Timu hiyo hufuata utaratibu mkali wa kutenganisha taka hatarishi, kama vile sindano, kondomu na vipande vya kioo vilivyovunjika, ambavyo hutibiwa katika eneo lililobainishwa na kupelekwa hospitali kwa utupaji salama.
Coco Beach imepata mabadiliko makubwa tangu mwaka 2017, wakati uchafuzi na kutelekezwa kulipokuwa tishio kubwa kwa bioanuwai na utalii. Mpango wa usafi wa Africraft uliamsha hamasa ya jamii na kuchochea msukumo mpya.
"Leo, fukwe ni safi zaidi, zenye mvuto zaidi, na zinatambulika zaidi kwa utalii wa mazingira," alisema Njovu. "Wageni na wafanyabiashara wanaiona kama eneo jipya la burudani na uwekezaji."
Africraft pia imepanua shughuli zake hadi shule za Dar es Salaam na Zanzibar, ambako wanafunzi hujifunza kubadilisha taka kuwa bidhaa zinazoweza kutumika.
Vipindi vya mafunzo katika Kituo cha WIM hujumuisha usafi wa fukwe na kutengeneza ndoo kutoka chupa na kutengeneza karatasi kutokana na karatasi zilizotupwa, na kupandikiza maadili ya uhifadhi wa mazingira kupitia mafunzo ya vitendo.
Warshteni ya shirika hilo karibu na Coco Beach imetengeneza zaidi ya bidhaa 400 kutoka kwa vifaa vilivyorejelewa, ikiwa ni pamoja na hereni kutoka kwenye maganda ya kahawa, vyombo vya mapambo vya kioo, na bangili zilizotengenezwa kutokana na nyavu za samaki zilizookotwa ufukweni. Bidhaa hizi huchochea biashara za ndani na kuonyesha ubunifu wa taifa.

Mpango wa Waste Changers sasa unahusisha jamii katika Zanzibar, Kigoma, Arusha, na mikoa ya Pwani. Zaidi ya wakazi 1,000 wamehusika, na mipango ya kupanua hadi mkoa wa Lindi inaendelea.
Kila eneo, Africraft huunganisha elimu, urejeshaji wa mazingira na uwezeshaji wa kiuchumi.
Kwa msaada wa Rosa Luxemburg Foundation, Africraft inatetea mfumo wa Extended Producer Responsibility, unaowawajibisha watengenezaji kwa taka zinazotokana na bidhaa zao baada ya matumizi.
Ingawa bado haujaingizwa rasmi katika sera ya kitaifa, Njovu na timu yake wanaendelea kushinikiza mabadiliko ya kimsingi.
Fukwe ambazo zamani zilikuwa zimejaa vipande vya kioo, nepi, na harufu mbaya sasa zimekuwa ishara ya ustahimilivu na ufufuo.
Jitihada zisizochoka za Africraft zimerudisha uzuri wa asili wa eneo hilo, kuamsha ushiriki wa wananchi, na kujenga jukwaa la mabadiliko ya mazingira yanayoongozwa na vijana.
"Coco Beach si safi tu," alisema Njovu. "Imejaa mawazo, vitendo, na mustakabali tunaoweza kujivunia sote."