Last Updated On 10 November 2020 1 Min Read
Uzani
Anerlisa apunguza uzani baada ya kubwaga kilo 14 ili kutoshana na marehemu dadake Tecra
Anerlisa amepunguza kilo 14
In Summary
Anerlisa ameichukua hatua hiyo ili kuziweka hai kumbukumbu za dadake
Anerlisa Muigai amekuwa akiwaonyesha mashabiki wake kuhusu anavyopiga hatua nzuri katika kupunguza uzani .
Amefichua jinsi alivyofaulu kubwaga kilo 14 kwa ajili ya kujitolea na bidii ya kuafikia lengo lake ili kutoshana kama alivyokuwa dadake Tecra .
Tecra aliaga dunia baada ya kuanguka na kupata majeraha mabaya kichwani Aprili tarehe 27 mwaka huu alipokuwa na mpenzi wake Lali Omar huko Lamu .
Lali mwenye umri wa miaka 54, alishtumiwa kwa kusababisha kifo chake na hata akafikishwa kortini . Alizikwa nyumbani kwao Naivasha mei tarehe 16 na kama hatua ya kuhaisha kumbukumbu zake ,dadake Anerlia ameamua kupunguza uzani ili atoshane na dadake