Ugomvi kati ya msanii wa bongo Alikiba na staa wa bongo Diamond Platnumz umeshuhudiwa kwa muda sasa na mashabiki wao.
Siku ya JUmatano Diamond Platnumz kupitia kwenye ukurasa wake wa instagram aliisuta kampuni ya Forbes kwa kumuweka kwenye orodha ya wanamuziki tajiri zaidi Afrika.
Mwanamuziki huyo tokea Tanzania aliwasihi Forbes kufanya utafiti dhabiti kabla ya kuweka jina lake kwenye orodha ya wanamuziki tajiri zaidi Afrika.
Baada ya Diamond kusuta kampuni hiyo, Alikiba kupitia kwenye ukurasa wake wa twitter alimsihi Diamond awache kulalamika kwani waliomuweka kwenye orodha hiyo wana akili ndefu.