26 May 2021 1 Min Read
ALISEMA NDIO!
Hongera Guardian Angel na Bi Esther Musila
Esther Musila, 51, akubali ombi la ndoa lake Guardian Angel, 30, siku ya kuadhimisha kuzaliwa kwake
In Summary
•Guardian Angel alimuomba ndoa Bi Esther Musila siku ya kuadhimisha kuzaliwa kwake
Mwanamuziki wa nyimbo za injili, Peter Omwaka almaarufu kwa jina la jukwaani kama Guardian angel kwa sasa ni mtu mwenye raha baada ya ombi la ndoa kukubaliwa na mpenzi wake Esther Musila siku ya kuadhimisha kuzaliwa kwake.
Kupitia mtandao wa Instagram, Guardian Angel,30, ametangaza kuwa Bi Musila alikubali ombi lake lililompata kwa mshangao akiadhimisha kufikisha miaka 51.
"NDIYO!! Asante sana mpenzi wangu.. aliondoka nyumbani akijua kuwa tumeenda kutia saini mpango wa biashara kisha ikawa mshangao wa siku ya kuzaliwa na kisha ikawa siku maalum sana maishani mwangu" Angel aliandika chini ya video inayoonyesha jinsi shughuli hiyo ya kufanya ombi la ndoa na kukubaliwa ilienda.
Wanamitandao wengi ikiwemo wasanii mashuhuri waliwapongeza wawili hao na kuwatakia maisha mema.
- Hongera
- Hongera
- Hongera
Angel na Musila wamekuwa kwenye uhusiano kwa kipindi cha mwaka mmoja sasa. Kutoka Radio Jambo, tunawatakia wapenzi hao ndoa yenye heri na upendo mwingi.