NI KWELI ALIIBA?
(+Video) Willy Paul atoa wimbo wa kumtusi Diamond Platnumz
Mwanamuziki huyo ambaye aligura sekta ya injili takriban miaka miwili iliyopita amekuwa akimkashifu Diamond kwa madai kuwa aliiba mawazo ya wimbo wake 'Nikune'
•Mwanamuziki Willy Paul ametoa wimbo wa kumtusi nyota wa Bongo Diamond.
•'Kamata, jicho kwa jicho, jino kwa jino" Paul alikuwa ameapa kwenye mtandao wa Instagram.
Mwanamuziki Willy Paul ametoa wimbo wa kumtusi nyota wa Bongo Diamond.
Willy Paul amekuwa akimkashifu Diamond kwa madai kuwa aliiba mawazo ya wimbo wake 'Nikune' ambao alishirikisha Nadia Mukami katika utunzi wa wimbo 'Kamata' ambao alitoa juzi.
Mwanamuziki huyo ambaye aligura sekta ya injili takriban miaka miwili iliyopita alikuwa ameahidi kuwa atatoa wimbo unaofanana na ule wa Diamond ili kulipiza kisasi.
'Kamata, jicho kwa jicho, jino kwa jino" Paul alikuwa ameapa kwenye mtandao wa Instagram.
"Simba, hakuna yeyote ambaye anamuibia mfalme. Nitakata kichwa chako" Willy Paul aliandika kwenye chapisho lingine kabla ya kutoa wimbo wake.
Hatimaye asubuhi ya Jumatano ametekeleza ahadi yake na kupakia wimbo uliojaa matusi yanayoelekezewa Diamond.
The video could not be loaded.
"Tusizoeane , kama mbaya mbaya! Mambo ya kuibiana mawazo na kuwa na dharau lazima iishe" Paul alisema.
Diamond aliachilia kibao kipya 'Kamata' siku tano zilizopita na ndicho kimeibua mzozo na Willy Paul.
The video could not be loaded.