In Summary
  • Ruth Matete afichua sababu ya kufunga kanisa la mumewe
Ruth Matete
Image: Ruth/INSTAGRAM

Baada ya mumewe msanii wa nyimbo za injili Ruth Matete kuaa dunia, msanii huyo hakuweza kuendelea na kanisa alililokuwa ameanzisha na mume wake.

KUlingana na Ruth, aifunga kanisa la mume wake kwani mumewe alikuwa na wito wa kuhudumia kanisa ilhali anajua hana neema ya kuhudumia kanisa.

Pia amefichua kwamba ananeema ya kusaidia na kuunga mkono kazi ya Mungu, na kabla ya kuoana na mumewe walijadili mambo yote kuhusu injili na kile kinachohitajika.

"Nilipokutana na mume wangu marehemu, Mchungaji Belovedjohn, alikuwa na nia sana kwa kusudi lake.

Alisema alitaka kuanzisha kanisa na kwamba alihisi kuongozwa na Mungu kufanya hivyo. Tulizungumzia mambo yote ya huduma kabla ya kuoa na nilijua ni nini nilikuwa najiingiza mwenyewe. Alikuwa na neema ya kuchunga kanisa. Sikuweza.

Lakini nilijua nilikuwa nimependelewa kumuunga mkono mchungaji. Kuna wanawake ambao wanaweza kuhudumia kanisa na kwa kweli wana neema yake.

Lakini najua sina hiyo neema. Ndio sababu wakati mume wangu alienda kuwa na Bwana, sikuendelea na kanisa ambalo tulikuwa tumeanzisha

Najua nafasi yangu kwa Mungu. Ninajua eneo ambalo nimepongezwa na kuitwa.

Nadhani ni muhimu tujue neema iliyo juu yetu. Kwa njia hiyo, hatutalazimisha vitu vyote kwa jina la huduma. Nilikuwa nikimuunga mkono mume wangu marehemu na huduma na ilikuwa inafanya kazi vizuri."

Ruth amefichua kwamba alimwambia mumewe kuwa hakuwa ameitwa na Mungu kuwa mchungaji wa kanisa.

"Nakumbuka wakati mmoja tulikuwa na mazungumzo waziwazi. Nikamwambia "Baby, sikuitwa kuwa mchungaji wa kanisa

Nimeitwa kwa soko. Tutafanyaje kazi pamoja na huduma hii ambayo Mungu ametupa?" Nakumbuka nikimwambia sitahubiri kwani sikudhani ningeweza kuhubiri

Nilidhani atakasirika. Lakini aliniambia anachohitaji tu ni msaada. Nilimuuliza awe maalum na aina ya msaada aliotarajia kutoka kwangu. Alisema vitu vichache," Ulisoma baadhi ya ujumbe wa Ruth Matete.

 

 

 

View Comments