In Summary
  • Khaligraph Jones akumbuka jinsi alifukuzwa jukwaani 2012
khali-e1471415170725

Khaligraph alitumia akaunti yake ya Instagram kukumbusha siku zake za mapema katika tasnia ya muziki.

Alikumbuka kuzomewa na kufukuzwa jukwaani mara moja.

Khaligraph Jones, ambaye kwa sasa ni mmoja wa wasanii wakubwa nchini, alikiri kwamba hakuwa msanii mzuri  au anayefahamika vyema wakati huo.

Alishiriki picha ya zamani akitumbuiza na kuwaburudisha mashabiki  katika Chuo Kikuu cha Limuru cha St Paul.

"Nilikaribia kuacha  muziki bana mnamo 2012, chuo kikuu cha St Paul ambapo nilizomewa na kufukuzwa jukwaani kama burukenge," Alisema Khaligraph.

Aliendelea kudai kuwa alitendewa vibaya kwa sababu hawakumheshimu kwa sababu OG hakuwa OG wakati huo.

"OG huyo hakuheshimiwa wakati huo kwa sababu OG alikuwa sio OG," akaongeza.

Khaligraph amepata hadhi yake ya OG kupitia kujitolea kwake kwa ufundi wake, na hakuna shaka kuwa yeye ni msanii mzuri.

 

 

 

View Comments