In Summary
  • Mbali na ugonjwa wake Akothee ameweza kumshukuru mumewe Nelly kwa kusimama naye wakati huu wa kipindi kigumu maishani mwake
akoth stylish 1 (1)

Mwanamuziki na mfanyibiashara mashuhuri Esther Akoth almaarufu kama Esther Akoth ameweka wazi kwamba bado anaendelea kupata nafuu kufuatia ugonjwa ambao umemwathiri kwa kipindi kirefu sasa.

Kupitia ukurasa wake wa Instagram, mwanamuziki huyo alifichua kuugua kwake kumemzuia  kufanya mambo mbalimbali aliyokuwa anafanya hapo awali.

Mama huyo wa watoto watano amesema katika kipindi hiki cha sikukuu hana uwezo wa kujiburudisha kwa njia mbalimbali ikiwemo kukata maji, kushiriki tendo la ndoa, kuenda kilabu pamoja na kupokea simu. 

Mbali na ugonjwa wake Akothee ameweza kumshukuru mumewe Nelly kwa kusimama naye wakati huu wa kipindi kigumu maishani mwake.

"Bado nitakuchagua wewe MFALME katika nafasi nyingine zozote 💋 Asante Bwana kwa zawadi ya uhai na mume mpendwa, sina cha kumpa baba Elizabeth @nellyoaks Mungu akubariki sana kwa kuchukua ujinga wangu 🙏

Hospitali ingekuwa gereza bila wewe. Nilikuwa na ulimwengu wangu, ambao ulinipa wakati rahisi wa kupona

Nitakulinda na kukupenda mradi tu Upendo wetu unalindwa kwa Damu ya Yesu 🙏. Ninaweza kuwa nimefikiria yote katika maisha yangu 🤔Lakini niamini kuwa utaanguka kwenye kifurushi kamili cha maisha yangu ❤️," Alisema Akothee.

Pia msanii huyo aliwashauri wanandoa na kuwaambia kuwa;

"Maneno yangu kwa Wanaume/wanandoa wote huko nje,Mpende anayekupenda, mpe uhusiano wako bora zaidi 🙏 Kamwe usilinganishe nyasi kwenye mtaa wako, nyunyiza maji kwa njia yako tu

Usiwahi kuwaumiza wale wanaokupenda, wanaweza wasikuumize tena, lakini wanaweza kuchagua kuondoka milele 💪 Asanteni sana mashabiki wangu kwa support, maombi ya upendo na kutoka kwa mashab

iki/marafiki na jamaa zangu. Tunakupenda pia Asante sana @premierhospke ❤️💋wewe ni bora💪 Bila @nellyoaks nani angekuwa nami hospitalini? Nani angeondoka ofisini kwake, mke, rafiki wa kike ili awe nami hospitalini kwa siku zote hizo? Ikiwa sio mtu anayenipenda na kunijali 🤔."

 

 

 

View Comments