'Nimemwachia Mungu pekee' Kusah aeleza kuhusu madai ya Ruby
•Mwanamuziki wa Tanzania Kusah amefunguka mazito baada ya mama wa mtoto wake Ruby kuzua madai kwamba alikuwa anatumia ushirikina wakati walikuwa wakiishi pamoja.
•Mimi sina mengi ya kuongea kwa sababu sio mara ya kwanza kwake kuongea maneno hayo
Mwanamuziki wa Tanzania Kusah amefunguka mazito baada ya mama wa mtoto wake Ruby kuzua madai kwamba alikuwa anatumia ushirikina wakati walikuwa wakiishi pamoja.
Wiki jana, Ruby alieleza yote yaliyokuwa yakiendelea baina ya wapenzi hao wawili hadi siku ambayo aliamua kutoka kwa ndoa yake.
Ruby ni msanii anayetambulika sana kwa sauti yake nyororo, walikosana na Kusah miaka miwili iliyopita na mwaka huu ndio aliamua kueleza yalitokea kwenye ndoa.
Kupitia kituo kimoja cha habari nchini humo, Kusah ameeleza kuwa Ruby, siku za hivi majuzi amekuwa akitumia ukurasa wa instagram kueneza uongo na kukiri kuwa yote aliyosema amemuachia Mungu.
"Mimi sina mengi ya kuongea kwa sababu sio mara ya kwanza kwake kuongea maneno hayo, tushamalizana ni miaka miwili sasa lakini tumebahatika kupata mtoto, kwa hiyo sisi ni wazazi, lakini ukiona mtu anathubutu kuandika ," alisema Kusah.
Alikana madai ya kupeleka Ruby kwa mganga huku akisema anayepaswa kujibu madai hayo ni Ruby na si yeye.
"Mambo ya kumpeleka Ruby kwa Mganga, yeye ndio kusema maneno, kwa hivyo sina mamlaka yakujibu,hata mkimuuliza yeye itakuwa ni kitu kizuri," alieleza.