"Hata miujiza huchukua muda kidogo" Muigizaji Celestine Gachuhi athibitisha ujauzito wa mtoto wa kwanza
•Gachuhi amepakia picha za ujauzito wake na kutaja hatua hiyo mpya kama muujiza uliochukua muda kutokea.
•Habari hizi zinakuja baada ya miezi kadhaa ya uvumi wa mashabiki ambao tayari walikuwa wamebaini ongezeko la tumbo la mwigizaji huyo.
Mwigizaji wa kipindi cha Selina Celestine Gachuhi na mpenzi wake mwanamuziki Phil Kimemia wamedhihirisha wazi kwamba wanatarajia mtoto wao wa kwanza.
Wanandoa hao wametumia siku ya Valentines kusherehekea mapenzi yao na kutangazia mashabiki kuhusu habari za ujauzito kupitia kurasa zao za mitandao ya kijamii.
Gachuhi amepakia picha za ujauzito wake na kutaja hatua hiyo mpya kama muujiza uliochukua muda kutokea.
"Hata miujiza huchukua muda mdogo" Gachuhi aliandika kwenye ukurasa wake wa Instagram.
Kimemia kwa upande wake amemsherehekea mkewe kama mwanamke jasiri aliyejawa na upendo, wema na ukarimu mwingi.
Mwanamuziki huyo amejivunia ukurasa mpya ambao wamefungua huku akimhakikishia mkewe kuwa atasimama naye kila wakati.
"Leo ikiwa ni siku ya Wapendanao, nimechagua kukusherehekea. Wewe ni mwanamke shupavu, mwanamke mrembo, anayejali, mpenzi mwenye upendo, msaidizi na mkarimu. Imekuwa safari nzuri na nimependa kila kitu! Huu ni ukurasa mpya na ghafla unajua tu ni wakati wa kuanza kitu kipya na kuamini miujiza ya mwanzo mpya. Nitakuwa upande wako wakati wote . Heri za siku ya wapendanao mpenzi Celestine Gachuhi" Gachuhi alisema.