In Summary

•Lengo la kampeni hizo ni kuhimiza Waafrika umuhimu wakujitokeza kwa wingi kupokea  chanjo dhidi Covid-19.

•Yemi atakuwa anazuru nchi za  Afrika  huku akitoa mwito kwa Waafrika na kuwaeleza umuhimu wa kupokea  chanjo ya kuzuia Corona.

Yemi Alade
Image: Hisani

Mwimbaji wa Nigeria Yemi Alade ameteuliwa kuwa balozi wa Afrika atakayekuwa miongoni mwa kikundi kitakachokuwa kinahimiza Waafrika kujitokeza kwa wingi  ili kupokea chanjo ya kujikinga na virusi vya Corona.

Lengo la kampeni hiyo ni kuhamasisha Waafrika kuhusu umuhimu wa kujitokeza kwa wingi kupokea  chanjo dhidi Covid-19.

Yemi atakuwa anazuru nchi mbalimbali  za  Afrika  huku akitoa mwito kwa watu kujitokeza na kuwaeleza umuhimu wa kupokea chanjo.

Yemi alieleza kuwa atatoa wimbo ambao maudhui yake yataangazia kampeni za kuhimiza Waafrika kujitokeza  kwa wingi kupokea chanjo ambazo zinapeanwa bila malipo.

"Ninafuraha kuwa sehemu ya #ItsUptoUs, vuguvugu hili linalohimiza Waafrika kuchukua jukumu la kufanya  ulimwengu kuwa salama tena. Nina furaha kutoa sauti yangu kwa suala hili muhimu na wakati huu,” alisema Yemi.

Mwaka jana kampeni za kuhimiza Waafrika kujitokeza kwa wiki kuchukua chanjo  zilifanyika katika nchi saba,Kenya ikiwa mojawapo ya nchi zilizofaidika na mafunzo hayo

View Comments