logo

NOW ON AIR

Listen in Live

Ommy Dimpoz afunguka alivyowekewa sumu nusura apoteze uhai

Dimpoz alikosekana kwenye sanaa kwa takriban miaka mitatu.

image
na Radio Jambo

Makala12 July 2022 - 04:05

Muhtasari


•Baada ya tukio hilo lilitokea 2018 Dimpoz alibaki akipambania uhai wake huku akifanyiwa oparesheni tatu maalum za koo katika juhudi za kuokoa maisha yake.

Ommy Dimpoz

Staa wa muziki Ommy Dimpoz amefunguka mbele ya mashabiki wake jinsi aliwahi kuwekewa sumu nusura apoteze uhai.

Baada ya tukio hilo lilitokea 2018 Dimpoz alibaki akipambania uhai wake huku akifanyiwa oparesheni tatu maalum za koo katika juhudi za kuokoa maisha yake.

Jumapili wakati akitumbuiza katika kipindi cha 'Break Point', Dimpoz aliimba "Sumu Waliniwekea, Bado Nusu Nikufuate Mama."

Hii inatafsiriwa kwamba  kwa sasa angekuwa marehemu, kwani ilibaki kidogo amfuate mama yake ambaye alitangulia.

Ommy Dimpoz ambaye ameuanza vyema mwaka huu huku tayari akiwa ameachia ngoma mbili, aliwahi kufichua kuwa tatizo la  koo lake lilitokana na sumu. 

Katika mahojiano na Millard Ayo, Ommy alifichua kwamba sauti yake ilirudi kabla ya kupelekwa nchini Ujerumani ambako alifanyiwa oparesheni ya tatu na ya mwisho.

Ikumbukwe, ni takribani miaka mitatu sasa imepita Dimpoz hakuonekana jukwaani akitumbuiza.

Jumapili Dimpoz alifanya tamasha yake ya pili ya  "Cheusi Cheupe" katika viwanja vya Zakhem, Mbagala jijini Dar es salaam.

Alishinda tuzo ya wimbo bora wa Kushirikiana mwakani 2012 kufuatia kibao alichoshirikisha  Ali Kiba.

Alianza kuimba akiwa shule ya msingi, lakini alipata tu kutunga wimbo wake wa kwanza alipokuwa shule ya upili.


RADIO JAMBO FREQUENCIES

Kisumu 100.1 | Mombasa 92.3 | Nakuru 96.9 | Eldoret 99.5 | Nyeri 99.3 | Nyahururu 97.3 | Webuye 95.3 | Meru 92.7 | Kitui 104.9 | Kibwezi 104.7 | Voi 105.7 | Malindi 98.1 | Lamu 104.7 | Narok 97.3 | Kapenguria 99.7 | Kisii 89.3 | Garissa 104.3 | Maralal 97.3 | Lodwar 92.7


logo© Radio Jambo 2024. All rights reserved