In Summary

•Akothee ameelezea kusikitishwa kwake na mwanafunzi aliyemdanganya kuhusu salio la karo yake ya shule na baadaye kutoweka bila maelezo.

•Akothee alifichua kuwa mvulana huyo alitembelea lango lake tena Ijumaa lakini hangeweza kuvumilia kumuona baada ya kumdanganya hapo awali..

Akothee, Woud Phoebe, Kiajana aliyerruka ndani ya boma lake.
Image: INSTAGRAM// AKOTHEE

Mwanamuziki na mjasiriamali Esther Akoth almaarufu Akothee ameelezea kusikitishwa kwake na mwanafunzi wa shule ya upili ambaye alimdanganya kuhusu salio la karo yake ya shule na baadaye kutoweka bila habari.

Katika taarifa ndefu siku ya Jumamosi, mama huyo wa watoto watano alisimulia jinsi mvulana huyo aliruka ndani ya boma lake Jumapili moja akiwa amevalia sare na kumsimulia matatizo yake.

Mvulana huyo alimsimulia jinsi alivyoamua kuchukua hatari ya kuruka ndani ya boma lake baada ya walinzi kumzuia kuingia langoni.

"Ilikuwa Jumapili asubuhi, Wuod Phoebe alikuwa akitembelea. Nilitembea hadi shambani na kuona mvulana aliyevaa sare za shule akiruka ndani ya boma langu. Kufuatia hilo nilimuuliza kwa nini hakupitia lango kuu bali aliamua kuruka ndani ya boma langu. Alisema, kuniona ni vigumu na walinzi wa lango hawakumruhusu kuingia, kwamba alikuwa amejaribu mara kadhaa,” Akothee alisimulia.

Aliendelea, "Basi, nilimuuliza, ingekuwaje kama alidhaniwa kuwa mwizi na kupigwa risasi au kujeruhiwa na mbwa au walinzi? Akajibu, ndiyo maana nilivaa sare yangu siku ya Jumapili, najua unajali elimu, nimesikia watu wakisema unalipa ada ya shule kwa wale wasio nayo , kwa hiyo niliamua kuchukua hatari. Kisha nikamuuliza, ulijuaje kuwa nipo kijijini? Alisema alinisikia nikizungumza katika mazishi karibu na kijiji hivyo akajua nilikuwa nyumbani.”

Mwimbaji huyo wa kibao ‘Simu’ alimuuliza kijana huyo salio la karo yake na akasema bado hakuwa amelipa Sh 20,000, ambazo alikubali kumlipia.

Isitoshe, mwanafunzi huyo alimweleza kuwa yeye ni mwanamuziki na baada ya kusikiliza baadhi ya muziki wake, mwimbaji Woud Phoebe ambaye alikuwa amemtembelea Akothee wakati huo alimshauri na kukubali kumsaidia kuanza kazi yake ya muziki baada ya kumaliza shule.

"Kisha nilimtuma mlinzi wangu shuleni ili kuondoa salio, mmm mvulana alidanganya, salio la ada lilikuwa 10k. Usalama wangu ulirejesha salio la muundo wa ada na risiti,” Akothee alisema.

Akothee alifichua kuwa mvulana huyo alitembelea lango lake tena Ijumaa lakini hangeweza kuvumilia kumuona baada ya kumdanganya hapo awali..

Kufuatia hayo, mwimbaji huyo aliwaomba ushauri mashabiki wake kuhusu  ni jambo gani sahihi la kufanya kwani alisikitishwa sana na mvulana huyo.

"Niliumia sana kujua kwamba alinidanganya na akanitenga. Sasa unadhani amerudi kwa ajili ya nini? Siwezi kuvumilia kumuona, ninahisi Kutumiwa. Ambacho wanangu huwa hawafanyi ni kunidanganya, naweza kukupiga mpaka usahau kupumua,ndio mimi ni mtia adabu. Je nimfungulie geti, nimpige kwanza kwa kudanganya kisha nimsikilize? Au arudishwe kwa mama yake?” aliandika Akothee.

Mwanamuziki huyo alionyesha picha ya mvulana huyo akiwa amesimama na Woud Phoebe na pia picha ya risiti aliyopewa baada ya walinzi wake kulipa ada.

View Comments