In Summary
  • Nyota huyo pia aliipongeza Kenya kuwa makazi yake ya pili, na kuongeza kuwa mtoto wake mmoja wa kiume amezaliwa na mama Mkenya.
Image: INSTAGRAM// DIAMOND PLATNUMZ

Staa wa bongo flava, Diamond Platnumz ameeleza ni kwanini mtoto wake aliyezaa na Hamisa Mobetto hakufuatana naye katika safari yake ya hivi majuzi nchini Rwanda ambapo alisafiri na watoto wa Zari Hassan na Tanasha Donna.

Mwimbaji ambaye alitua nchini kwa  ajili ya kutumbuiza mashabiki katika hafla ya Oktobafest alielezea kuwa haiwezekani kuenda  pamoja na watoto wake wote kila mahali anapoenda kwani hii inaweza kuvuruga maisha yao.

Diamond alidokeza kuwa wakati wa safari yake nchini Rwanda kwa ajili ya Tuzo za Trace Gala, Dylan alikuwa shuleni.

“Sio kila sehemu ni vyema kwenda na watoto, ndiyo maana nilikuja hapa peke yangu, kwa wakati unatakiwa kuwaacha kusoma.

“Kwa hiyo nilikwenda nao Rwanda lakini hapa nilikuja peke yangu kwa sababu watoto wako shuleni na wakati mwingine si vyema kwenda nao kila mahali. Nitaziharibu,” Diamond alieleza waandishi wa habari.

Diamond aliibua sintofahamu baada ya kuingia Kigali na watoto wake watatu.

Nillan, Tiffah na Naseeb Junior waliongozana na baba yao hadi Kigali huku Dylan akiwa hayupo kwenye picha, huku mashabiki wakihoji kutokuwepo kwake baada ya kushiriki video hiyo.

Nyota huyo pia aliipongeza Kenya kuwa makazi yake ya pili, na kuongeza kuwa mtoto wake mmoja wa kiume amezaliwa na mama Mkenya.

“Kenya ni kama nyumba ya pili kwangu hasa tangu mtoto wangu mdogo (Naseeb Junior) azaliwe hapa. Najisikia nyumbani kweli. Nchi imekuwa na mchango mkubwa katika kusaidia kazi yangu ya muziki kupitia matukio mbalimbali hivyo nina mapenzi makubwa na Kenya.” Alisema Diamond.

Alionyesha hisia ya kuhusika na kuthamini uungwaji mkono mkubwa ambao amepokea kutoka kwa Wakenya ambao umepeleka taaluma yake katika kiwango kingine.

Mwimbaji huyo alikuwa sehemu ya kikosi kilichojaa nyota kwa ajili ya Tusker OktobaFest katika uwanja wa Ngong Racecourse.

 

 

 

 

 

View Comments