In Summary

•Mulamwah alichapisha video iliyomuonyesha akiwa kwenye kituo cha treni ambapo alionekana akijaribu kusimamisha treni.

•“Of course I am a toxic baby mama, nilimwambia binti yangu kuwa babake aligongwa na treni akiwa kazi ya reli," Sonie alisema.

Mulamwah na ex wake Carrol Sonie
Image: INSTAGRAM// MULAMWAH

Mchekeshaji David Oyando almaarufu Mulamwah amejibu kwa utani baada ya aliyekuwa mpenzi wake, Caroline Muthoni kukejeli uhusiano wao wa sasa na ushirikiano katika malezi.

Katika video ya hivi majuzi, Bi Muthoni ambaye anajulikana sana kama Carrol Sonie alikejeli uhusiano kati yake na mzazi huyo mwenzake wakati akijibu video ambayo Mulamwah alikuwa amefanya hapo awali.

Miongoni mwa madai ambayo muigizaji huyo aliibua kwenye video hiyo ni kwamba alimwambia bintiye kuwa baba yake aligongwa na treni alipokuwa akifanya kazi kwenye shirika la reli.

“Of course I am a toxic baby mama, nilimwambia binti yangu kuwa babake aligongwa na treni akiwa kazi ya reli. Of course I am a toxic baby mama, mimi ndiye hupatia baby daddy content, he cannot do without me,” Carrol Sonie alisema kwenye video yake.

Pia alisema, “Of course I am a toxic baby mama, ata ex akinitext na pseudo account eti ananimiss, ata hiyo nablock. Ofcourse I am a toxic baby mama ‘Keilah is not my kid’ ataendelea kumuonea mitandaoni.”

Katika kile kilichoonekana kama jibu lisilo la moja kwa moja kwa muigizaji huyo, Mulamwah alichapisha video iliyomuonyesha akiwa kwenye kituo cha treni ambapo alionekana akijaribu kusimamisha treni.

"Trainee, February ina mengi ikiwa ni pamoja na fainali ya AFCON," Mulamwah alisema kwenye sehemu ya maelezo ya video hiyo.

Katika video hiyo aliyoichapisha kwenye Instagram, mchekeshaji huyo mwenye umri wa miaka 31 alionekana kutotulia na mwenye mawazo wakati treni ilipokuwa ikikaribia alipokuwa amesimama.

Makumi ya watumiaji wa mtandao wa Instagram tangu wakati huo wamejibu video hiyo huku wengi wakionekana kuihusisha na madai yaliyotolewa na Carrol Sonie hapo awali.

Soma maoni kutoka kwa baadhi ya wanamtandao;-

Sir_p.h.i.l.l: Babake ameenda agongwe na train ya ukweli.

Sybilisibo: No wonder she said bila yeye huna content, it’s true now.

Tonymwenda254: Hapa ni before ama after imekugonga.

Marione_tobbias: Enyewe sonie anakupea content vile alisema.

Masterclassic_: Hapa ndio uligongewa.

Moragwal_ke: Umeamua iwe reality ugongwe na train.

View Comments