In Summary

•Akothee alizungumzia jinsi ambavyo bado wamejipata pamoja licha ya kujaribu kuachana katika siku za nyuma na hata kujaribu mahusiano mengine.

•Aliwaonya wale wanaojaribu kuchumbiana naye au Nelly Oaks baada ya kutengana, akiwasihi wasiwe na raha katika uhusiano huo.

 

"Tumejaribu kuachana, tumejaribu kwingine, tukakosa amani tukarudiana!" Akothee azungumzia mahusiano na Nelly Oaks

Akothee na aliyekuwa mpenzi wake Nelly Oaks
Image: INSTAGRAM// AKOTHEE

Mwimbaji na mjasiriamali mashuhuri wa Kenya Esther Akoth almaarufu Akothee amefichua baadhi ya masuala mazito kuhusu uhusiano wake na Nelly Oaks.

Katika taarifa yake ya siku ya Jumapili, mama huyo wa watoto watano alimsherehekea mwanamume huyo maalum katika maisha yake alipokuwa akiadhimisha siku yake ya kuzaliwa na kutumia fursa hiyo kufunguka kuhusu jinsi wanavyopendana.

Akothee alizungumzia jinsi ambavyo bado wamejipata pamoja licha ya kujaribu kuachana katika siku za nyuma na hata kujaribu mahusiano mengine.

"Kheri ya siku ya kuzaliwa osiepna. Osiepnani bende oseyuare koda ndi. Wanafiki ,josem , tumejaribu kuwachana, tuka kimbia tukajaribu kwingine, sote tulikosa amani huko tumerudi," Akothee alimwandikia Nelly Oaks kupitia mtandao wa Instagram.

Aliongeza, "Hatujui jinsi ya kuachana. Tunachojua ni jinsi ya kurudi pamoja. Nadhani sisi sote ni SUMU 🤣🤣🤣. Hii ndiyo maana halisi ya uhusiano wenye sumu.”

Mwanamuziki huyo mwenye umri wa miaka 43 aliendelea kuwaonya wale wanaojaribu kuchumbiana naye au Nelly Oaks baada ya kutengana, akiwasihi wasiwe na raha katika uhusiano huo kwani kuna uwezekano wa wao kuachwa wakati wowote.

"Ikiwa utaingia kwenye uhusiano na yeyote kati yetu ndani ya miezi 6 ya mapumziko yetu, usitulize kichwa chako hapo. Siku tukikutana kwenye tamasha au popote pale, utawachwa kwa mataaaaaa. Sisi pia hatujui kwanini? Hatuhoji hata kilichotokea,  baadhi yetu tulipiga hatua kubwa kwa kuwa msichana mkubwa, kiliniramba kweli kweli 🤣🤣🤣," alisema.

Pia alitangaza kwamba hatagura uhusiano na meneja wake tena, hata wakati kutoelewana kunatokea.

"Sasa sitaita kutokuelewana kwetu kuwa ni kuvunjika, nitajaribu kufanyia kazi uelewa wetu mdogo ikiwa kutoelewana hakufanyi kazi. Safari hii, sipangi virago, nitaenda naye. Madam Pack na usiende mahali popote. Mapenzi niue. Kijana ni wangu. Shoneni vitenge,” alisema.

Akothee alirudiana na mwanamume huyo ambaye pia ni meneja wake, katikati mwa mwaka jana, miezi michache tu baada ya ndoa yake na Denis Schweizer kuvunjika.

View Comments