Fikra za Bahati
Je, Bahati ameacha injili? Tazama kibao chake kipya
Kwenye kibao hicho, Bahati amesikika akiwadhalilisha wasanii wengine kama Sauti Saul, Ringtone, Khaligraph na Octopizzo.. Khaligraph amjibu
•"Alafu naskia Bahati ameanza bangi na sigara ameanza kurap matusi, punguza iyo bangi baba wacha kiherehere" Khaligraph alimjibu Bahati.
•Kwenye video hiyo, Bahati pia anaonekana kwenye klabu akivuta sigara kubwa
The video could not be loaded.
Kwenye kibao hicho, Bahati amesikika akiwadhalilisha wasanii wengine kama Sauti Saul, Khaligraph na Octopizzo.
Picha za video hiyo zilizokuwa zimeonyeshwa kabla ya video kuachiliwa na ambazo zilionyesha Bahati akivuta sigara kubwa zilikuwa zimeibua hisia mbalimbali miongoni mwa Wakenya huku ikisemekana kuwa huenda msanii huyo ameiaga injili.
Ringtone ni mmoja wa wasanii waliomkahifu Bahati huku akisema kuwa Bahati alikuwa ameacha injili na kuingilia utumizi wa madawa ya kulevya.
Khaligraph ambaye kwa sasa ako katika ziara nchini Marekani amemjibu Bahati huku akimwambia awache bangi na apunguze Kiherehere.
"Alafu naskia Bahati ameanza bangi na sigara ameanza kurap matusi, punguza iyo bangi baba wacha kiherehere" Khaligraph alimjibu Bahati.