Msanii kutoka Tanzania, Harmonize amempigia magoti Madam Rita kama njia moja ya kutoa shukran zake kwa kumsaidia kujenga kipaji chake.
Hili lilitokea katika hafla ya Serengeti Festival iliyofanyika mjini Dodoma, huku Harmonize akionyesha hisia nyingi jukwaani.
“Sio lazima mtu akuambie yes ndo usaidike, anaweza akakuambia no na akawa amekusaidia. Niseme kweli, hakungekuwa na Kondeboy bila Madam Rita,” Harmonize alisema.
Vilevile aliwarai vijana wote kutokata tama badala yake kuzidi kujituma maadamu wana kipaji na wanaamini kwamba siku moja watafanikiwa.
Kuna asilimia ya mashabiki waliokuwepo kwenye hafla hiyo ambao hawakupenda kitendo cha ‘Jeshi’ kumpigia Rita magoti ila baadhi pia walikubaliana nacho wakisema ilikuwa ishara nzuri ya kutoa shukurani.