In Summary
  • Hapo awali kwenye mitandao ya kijamii, alitangulia kuwaambia mashabiki wake kwamba ameamua kuacha kunywa pombe
Thee Pluto
Image: INSTAGRAM

Thee Pluto  ni mfanyabiashara na mtayarishaji wa maudhui youtube na tiktok kwa kuwa yeye ni mtu mashuhuri na mhusika wa mitandao ya kijamii.

Amekuwa na sehemu yake ya kashfa zinazohusu vipindi vyake vya mtihani wa uaminifu kwenye youtube kwani amekuwa akishutumiwa mara nyingi kwa kuandika kipindi hicho.

Pia ameshutumiwa kupata utajiri wake kwa kuwalaghai watu mtandaoni na mwanablogu xtian Dela na Andrew Kibe.

Kwa kawaida Pluto anafahamika kwa kuishi maisha yake ya kifahari,hivi majuzi muunda maudhui huyo alibarikiwa na kifungua mimba wake.

Hapo awali kwenye mitandao ya kijamii, alitangulia kuwaambia mashabiki wake kwamba ameamua kuacha kunywa pombe.

Kulingana naye, kila anapocheza klabu, watu wanapaswa kuacha kumnunulia pombe na badala yake wamnunulie Delmonte au hata maji.

Kulingana naye, wakati wake kama mnywaji pombe umefika mwisho.

"Mi huingia club napatana na fan mmoja anasema Pluto itisha anything nitalipa,ata kama sikuwa nilewe nalewa, uki iona this time niitishie DElmonte ama maji,wakati wa kuwa mlevi umefika mwisho,"Aliandka Pluto.

 

 

 

View Comments