In Summary

• Mrembo huyo alisema kwamba alimpokea Yesu na kudokeza kuwa alibatizwa siku ya kusherehekea kuzaliwa kwake Mei mwaka jana.

• Akisimulia kupata wokovu, Chyna alisema kwamba sauti ilimjia ikimtaka kufahamu kusudi lake katika maisha.

Blac Chyna afuta tattoo ya kishetani, amkimbilia Mungu
Image: Instagram

Mwanamitindo wa Marekani, Blac Chyna ambaye kwa muda mrefu alijizoelea umaarufu kutokana na taswira yake ya kuvutia na mwonekano wa kupita kiasi aliopata kwa upasuaji wa plastiki na vijazaji, hatimaye ameasi muonekano huo.

Katika mahojiano ya kipekee na kituo cha runinga cha Fox News, Chyna, ambaye jina lake halisi ni Angela White, alisema yeye ni Mkristo aliyezaliwa mara ya pili - na anafanya mabadiliko makubwa katika maisha yake ili kuakisi hilo.

Moja ya mabadiliko hayo, kama alivyoeleza kwenye video mpya aliyoshiriki kwenye Instagram, ni kuondolewa kwa tattoo ya “kishetani” kwenye nyonga yake.

"Kwa hivyo mnajua kwamba nilipata tattoo hii ya Baphomet," alisema, akimaanisha mungu wa zamani wa kipagani ambaye anaonyeshwa kama mbuzi mwenye pentagram kwenye paji la uso wake na kwa kawaida anahusishwa na Shetani.

"Inabidi iondoke, unajua ninamaanisha nini?" Aliuliza. "Mimi si karibu kuwa na alama ya mnyama, hakuna kitu kama hicho."

Chyna aliongezea, "Nitawaambia hivi, nilipochora tattoo hiyo mara ya kwanza, sivyo ilimaanisha kwangu, unajua ninamaanisha nini? Bila kujali ni nini, sitaki tu chochote hasi au kishetani tena."

Itachukua vipindi kadhaa ili kuiondoa kikamilifu, lakini inaonekana kwamba Chyna amefurahi kuchukua hatua hii, ambayo ni moja tu ya mabadiliko ambayo amekuwa akifanya katika maisha yake hivi majuzi, Fox waliripoti.

Kando na kufuta tattoo hiyo ya kishetani, Chyna pia Ameondolewa vipandikizi vya matiti na vipandikizi vya gluteal, na vile vile ameondolea vishimo alivyoweka kwenye mashavu yake.

Pia ameachana na akaunti yake ya OnlyFans yenye mafanikio makubwa ambayo ilikuwa inauingizia mamilioni ya pesa.

Chyna hivi majuzi alijadili maamuzi haya kwenye kipindi cha "Fox and Friends Weekend," akieleza, "Kusema kweli, kwangu, nilikuwa kama, hii ni nyingi sana. Ni wakati wa mabadiliko. Hii sio mimi ni nani. Kitu kilinijia kama , Roho Mtakatifu alikuja juu yangu. Na nikasema, 'Unajua nini? Nahitaji kufahamu kusudi langu maishani. Kama, kwa nini niko hapa?'’

Chyna pia hivi majuzi alienda kwenye Instagram kushiriki kwamba alibatizwa kwenye siku yake ya kuzaliwa Mei iliyopita.

“Nilibatizwa tarehe 5-11-22 ….. Nilikuwa nikitazama video tena na nilitaka kuwaonyesha hili kwa sababu mkichunguza kwa makini mdomo wangu unaweza kusikia roho zikiondoka kwenye mwili wangu,” alinukuu video hiyo, "Mungu ni mwema".

View Comments