In Summary

• "Mwanamume atampenda mwanamke hadi kuzimu, lakini labda yuko mahali fulani, na uume wake unaamua tu kitu cha kujamiiana nacho,” 2Baba alisema.

• Mwezi Agosti mwaka jana, Annie alimsamehe mumewe 2Baba baada ya kukiri kupata mtoto wa 6 nje ya ndoa yao.

2baba akiri kuwa wanaume wote wameumbwa kuwasaliti wake zao katika mapenzi.
Image: Instagram

Mwimbaji mkongwe wa Nigeria, Innocent Idibia, almaarufu 2Baba, amesema kuwa wanaume wameumbwa kudanganya na kuchepuka baada ya kumsaliti kimapenzi mkewe mara nyingi.

Mwimbaji huyo alisema haya katika msimu wa hivi punde zaidi wa mfululizo wa uhalisia maarufu "Young, Famous & African" mbele ya mke wake, Annie, na nyota mwenzake, Nadia Nakai.

Mbele ya mke wake, mwigizaji Annie Idibia, alieleza kuwa matamanio ya wanaume ni ya silika na kimsingi yanasukumwa na hamu ya kutosheleza ngono.

2baba alisema kwa sauti ya hakikisha akisisitiza kwamba wanaume siku zote tabia yao ni ya kuchepuka kwa sababu waliumbwa hivo na mifumo ya miili yao ndivyo ilivyo na hivyo wanawake hata wakatuama vipi hawawezi kushindana nao wakaweza.

Alisema, “Mpende msipende, wanaume wameunganishwa hivyo. Mwanamume atampenda mwanamke hadi kuzimu, lakini labda yuko mahali fulani, na uume wake unaamua tu kitu cha kujamiiana nacho,” 2Baba alisema.

Nadia, mshiriki wa onyesho hilo, kisha akaingilia kati, akisema si sehemu za siri za mwanamume huyo bali ni akili yake inayofanya maamuzi kama hayo, ambapo 2Baba alijibu, “Sawa, haijalishi jinsi gani utaliangazia hilo, ukweli ni kwamba mwanamume atajamiiana nje ya ndoa tu,”

Akijibu, Annie alihoji mume wake ikiwa maoni yake yaliakisi imani yake ya kibinafsi au taarifa ya jumla.

Kujibu, 2Baba alibaini kuwa ilikuwa imani na maoni yake binafsi juu ya suala hilo.

 Hata hivyo, sehemu ya watumizi wa mitandao ya kijamii

View Comments