In Summary

• Rocky alisikika akiwafokea kwa kukerwa huku akiwataka wote kuonesha tabia za kiutu uzima ndani ya ukumbi huo wa starehe.

• Wawili hao walifichua jina la mtoto wao wa kwanza hivi majuzi wakati wa kumsherehekea kufikisha mwaka mmoja.

Rocky awafokea walevi kupigana mbele ya mkewe Rihanna
Image: Instagram

Msanii A$AP aliwafokea vikali walevi katika klabu ya starehe ambao walizua fujo na kutishiana kurushiana ngumi mbele ya mkewe mjamzito, Rihanna.

Katika video inayosambaa mtandaoni, rapper huyo anasikika akikasirishwa na wahudhuriaji wa kilabu cha usiku baada ya kupata ugomvi karibu na mpenzi wake aliyeshinda tuzo ya Grammy wakati wa matembezi ya hivi majuzi.

Rocky alisikika akiwafokea kwa kukerwa huku akiwataka wote kuonesha tabia za kiutu uzima ndani ya ukumbi huo wa starehe.

"Nyinyi wote fanya kama waungwana hivi sasa, mmesikia?" Alisema Rocky, 34, kwenye kipaza sauti kwenye eneo lenye mwanga hafifu. "Niko humu ndani ya mke wangu."

Aliendelea, "Nyie hebu tuliza kabisa hizo pumba zetu, kila mtu. Msiwe katika sehemu hii kufanya upuuzi wenu. Tulia na nyinyi wote kuweni kama waungwana wakati nyote mpo mbele yetu."

Mapema mwezi huu, nyota hao ambao kwa sasa wanatarajia mtoto wao wa pili - walisherehekea mtoto wao RZA Athelston siku yake ya kuzaliwa kwa jukwa la picha mbalimbali za familia.

A$AP alianza chapisho na picha nzuri ya RZA akitambaa kwenye blanketi karibu na msanii nyota, 35, huku akimbusu A$AP Rocky kwenye shavu. Pia alishiriki picha zingine nyingi za watatu hao wakionyesha kamera na kufanyiana utani kwenye kioo.

Kisha alichapisha picha kadhaa za yeye akishirikiana na mwanawe, ikiwa ni pamoja na picha yake akinyoa na RZA mikononi mwake na hata video ambapo baba mwenye fahari anamshikilia mwanawe juu na kucheza naye karibu.

Slaidi yake ya mwisho ya chapisho ilionyesha video ya mwanachama mwanzilishi wa Ukoo wa Wu-Tang Ol' Dirty Bastard kwenye onyesho la tuzo akisema kwamba "Ukoo wa Wu-Tang ni wa watoto."

Jina la kipekee la mtoto wa kiume lilithibitishwa na cheti cha kuzaliwa kilichopatikana na majarida mbalimbali mapema mwezi huu.

Jina linatoa heshima kwa kiongozi wa Ukoo wa Wu-Tang, mtayarishaji na rapper RZA (tamka "Rizza"), ambaye jina lake halisi ni Robert Fitzgerald Diggs.

Jina hilo lilikuja karibu mwaka mmoja baada ya mwimbaji huyo wa "Diamonds" na Rocky kukaribisha mtoto wao wa kwanza pamoja na miezi michache tu baada ya Rihanna kuushangaza ulimwengu kwa ujauzito wa pili wakati wa show yake  ya Super Bowl.

View Comments