Mwimbaji wa nyimbo za injili Kambua amefunguka kuhusu malezi na kufichua kumpoteza mtoto mwingine.
Katika video aliyoshirikishwa kwenye chaneli yake ya YouTube, mwimbaji huyo alifichua kuwa hajawahi kutangaza habari hiyo hadharani.
"Wengi wenu mnajua kuwa nina watoto watatu, Nathaniel, Malaki ambaye yuko mbinguni, na Natalie. Lakini ukweli ni kwamba nina watoto wanne. Hiki ni kitu ambacho sijawahi eleza umma, lakini nadhani ni wakati wa kukuleta katika ulimwengu wangu na kukuambia juu ya watoto wawili ambao waliaga na wawili ambao nalea," alisema.
Kambua hakufichua ni lini hasa alimpoteza mtoto wake mwingine kwani sehemu ya kwanza ya hadithi iliangazia zaidi uhusiano wake na baba yake najinsi alivyokutana na mumewe.
Mnamo Februari 2021, mwimbaji huyo wa nyimbo za injili alitangaza kuwa amempoteza mwanawe , Malachi.