In Summary

• Baada ya Drizzy kugeuza ngoma, aliingiza mkono wake ndani na kuchimba huku na kule huku umati ukishangilia, alitangaza mshindi kuwa mwenye tikiti nambari "17482."

Drake
Image: Instagram

Rapa maarufu kutoka nchini Kanada amewakosha mashabiki wake baada ya kumpa mmoja wa mashabiki wake gari la kifahari aina ya G Wagon wakati wa shoo yake mjini Toronto, Kanada.

Rapa huyo mwenye umri wa miaka 36 alipokuwa akitumbuiza kwenye tamasha lake la 'It's All a Blur Tour' katika uwanja wa Scotiabank Arena katika mji wake wa asili, Toronto siku ya Jumamosi, alitoa zawadi ya Mercedes-Benz G-Wagon kwa shabiki asiyetarajia.

Badala ya kuchagua binafsi shabiki kwenye hadhira ya kwenda nyumbani na zawadi ya kifahari, Drake aliyefika kwa shoo hiyo akiwa amejipanga aliamua kuchagua ngoma ya bahati nasibu ambayo ilikuwa na nambari za tikiti za kipekee za waliohudhuria.

"Kwa hivyo, hivi ndivyo nitafanya: nitachagua tikiti ya ushindi kutoka kwa ngoma hii hapa," Drake alisema, wakati washiriki wa timu yake wakileta ngoma ya bahati nasibu kwenye jukwaa. "Nataka kila mtu awe kimya sana. Nataka kusikia mshindi akipiga kelele.”

Baada ya Drizzy kugeuza ngoma, aliingiza mkono wake ndani na kuchimba huku na kule huku umati ukishangilia, alitangaza mshindi kuwa mwenye tikiti nambari "17482."

Hatimaye, alimwona shabiki aliyekuwa akipeleka gari jipya nyumbani katika moja ya ngazi za juu za Scotiabank Arena.

Ipasavyo, alisema, "Wamezipata? Wao juu? Bora ulete punda wako hapa. Tutamtuma mtu huko aangalie tikiti hiyo."

Hata hivyo haijulikani ni modeli gani ya Mercedes-Benz G-Wagon ambayo msanii wa "Rich Flex" alitoa lakini kulingana na tovuti ya Mercedes-Benz, modeli ya kawaida inauzwa kwa $139,900 sawa na shilingi za Kenya 20,831,110.

Tazama video hii jinsi msanii huyo alifanya kufuru hiyo ambayo haijawahi tokea kwenye tamasha loote duniani;

View Comments