In Summary

• Baunsa huyo wa Kizz Daniel kwenye video akishiriki mchezo wa ndondi na mwanamume huyo na ilisababisha mwanamume huyo kukaribia kupoteza maisha katika mchakato huo.

Baunsa wa Kizz Daniel
Image: Screengrab//InstagramVideo

Katika siku za hivi karibuni, baunsa wa msanii wa Afrobeats Kizz Daniel anayefahamika mitandaoni kama Kelvin Power amekuwa gumzo la mitandaoni baada ya kuonekana hadharani kwa mara ya kwanza mwishoni mwa mwaka jana.

Kelvin Power baada ya kuonekana akizungumza kwa mara ya kwanza na waandishi wa habari za mitandaoni, umaarufu wake uliongezeka hata Zaidi mpaka kuangukia dili la ubalozi wa mauzo na kampuni moja ya biashara.

Baada ya umaarufu huu, jamaa mmoja alijitokeza na kumualika kuingia naye katika mduara kwa pambano la ngumi.

Pambano hilo lilifanyika mwanzoni mwa mwaka huu na video kutoka kwa pambano hilo imefanya mlinzi huyo wa Kizz Daniel kuwa gumzo mitandaoni baada ya kuonekana akimnyeshea ngumi za kila rangi bila huruma jamaa huyo.

Baunsa huyo wa Kizz Daniel kwenye video akishiriki mchezo wa ndondi na mwanamume huyo na ilisababisha mwanamume huyo kukaribia kupoteza maisha katika mchakato huo.

Bila kujitahidi, mlinzi wa Kizz Daniel alipiga ngumi nzito kwa mpinzani wake na kusababisha mpinzani kupoteza usawa wake kila wakati.

Alijaribu kumpiga mpinzani ngumi nyingine ili apate kipigo lakini mwamuzi akapima uzito ili kuzuia hatari ya mpinzani.

Kelvin Power aligonga vichwa vya habari mwaka wa 2023 kufuatia jinsi anavyochukulia kazi yake kwa uzito kila anapokuwa na mwimbaji huyo kwenye hafla.

Jinsi alivyomlinda mwimbaji huyo dhidi ya mashabiki waliokuwa na bidii kupita kiasi alipokuwa jukwaani kulisababisha umaarufu wake mtandaoni.

View Comments