In Summary

β€’ "Usiruhusu kitumbo chako kukuzuie kuchapisha video hiyo kwenye simu yako! Ichapishe tu,” aliandika.

Yemi Alade
Image: Instagram

Jumbe za pongezi zimeanza kumiminika katika ukurasa wa Instagram wa mwimbaji na mtunzi maarufu wa Nigeria Yemi Alade kufuatia video yake mpya iliyosambaa mtandaoni.

Yemi Alade mwimbaji maarufu wa "Jhonny" alishiriki video ya kiashiria cha kuwa na ujauzito wake akikua kupitia ukurasa wake wa Instagram uliothibitishwa leo, Januari 3, 2024.

Kumbuka kwamba Yemi Alade, mama mjamzito mwenye umri wa miaka 34 amekuwa akihusishwa kuwa kwenye uhusiano na meneja wake wa muda mrefu Taiye Aliyu.

Katika video hiyo mpya ya Instagram, Yemi Alade licha ya kuwa na mtoto mchanga anaonyesha ustadi wake wa kucheza.

Mwimbaji huyo aliinua nyusi wakati anacheza na wimbo wake mpya wa Amazing Grace."

Katika maneno ya kuambatanishwa kwenye video hiyo, Alade mwenyewe alionekana kudokeza kwamba huenda ana mimba kweli baada ya kusema kwamba asingeacha tumbo lake linalokua kumzuia kutokatika densi.

β€œHeri ya mwaka mpya 2024 Wapendwa wangu! 🍾 πŸ₯‚ πŸŽ‰ Usiruhusu kitumbo chako kukuzuie kuchapisha video hiyo kwenye simu yako! Ichapishe tu,” aliandika.

Hizi hapa ni baadhi ya jumbe za hongera kutoka kwa mashabiki wake waliofurahishwa na hiyo video;

paul1npat: Je, yeye ni mjamzito? Itakuwa habari njema.

corazchep: Yemi ni mjamzito ujumbe upo kwenye pakiti moja πŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™ŒπŸ™Œ.

loladaayes: Ndiyo mkuu, nitaisukuma kwa fahari 😍.

__veevianne: Mama tunatarajia mii kidogo ❀️.

View Comments