In Summary

• Betty Kyallo amefichua kuwa yuko kwenye uhusiano ambao unaweza kumwona akiolewa hivi karibuni.

•"Nikikupenda nafanya kila kitu. Napika, nakupigia magoti, massage nakufanyia. lakini yote ni kama nakupenda. Kama sikupendi siwezi fanya izo vitu zote," alisema.

Image: INSTAGRAM// BETTY KYALLO

Katika mahojiano ya hivi majuzi, Betty Kyallo alielezea furaha yake baada ya kurejeea kwenye kazi ya uanahabari baada ya miaka nne.

 Betty Kyallo amefichua kuwa yuko kwenye uhusiano ambao unaweza kumwona akiolewa hivi karibuni.

Mama huyo wa mtoto mmoja alifichua kwamba yuko kwenye uhusiano na anafurahia mahusiano yake ya sasa.

“Sasa nimetulia. Nasikia furaha,” Betty alieleza.

Alipoulizwa kuhusu harusi hivi karibuni, “Tutaona kuhusu hilo. Sitaki kuongea mengi juu yake halafu kitu kitokee."

Pia alifichua kwamba ilikuwa bora zaidi kuchumbiana katika miaka ya thelathini.

"Wanawake wa miaka thelathini tunatengeneza washirika wazuri sana katika uhusiano kwa sababu tuna uzoefu mwingi. Tumepitia mengi maishani.”

Betty alikiri kwamba kwa mwanamume anayempenda, huwa mtiifu sana.

“Nikikupenda nafanya kila kitu. Napika, nakupigia magoti, massage nakufanyia. lakini yote ni kama nakupenda. Kama sikupendi siwezi fanya izo vitu zote

Hata hivyo, maisha yake ya mapenzi yana sehemu yake nzuri ya upendo na chuki mtandaoni, na Betty anakiri kuwa ni vigumu kuangazia hili kama mtu mashuhuri.

“Unajua nimekuwa nikifanya hivi kwa miaka 13 sasa. Nimejifunza mengi kwa sababu baadhi ya mambo ambayo watu hupitia faragha mimi hupitia hadharani. Sio rahisi lakini natafuta njia za kupita."

View Comments