In Summary

• Katika video hiyo, anaonekana akiwaburudisha waliohudhuria katika mapokezi hayo.

• Tukio hilo lilikuwa la furaha huku umati wa watu wakifurahia chakula, muziki na sherehe.

Karamu ya harusi
Image: Instagram

Kizaazaa kilishuhudiwa katika karamu ya harusi moja baada ya mfawidhi wa karamu hiyo kuwafokea wageni akidai wamekula chakula kingi.

MC huyo alionekana akiwakaripia wanaume waliokuwa wameketi wakisasambua minofu na nyama katika karamu hiyo.

Alisikika akimuonya mwanadada aliyekuwa akiwapakulia wageni vyakula dhidi ya kuwapakulia wanaume hao akiwauliza tangu wafike katika katramu hiyo ni mara ngapi wamekula.

“Usimuongezee chakula huyo mwanaume, hebu nikulize wewe mwanaume, wewe ndiye umefadhili hii karamu? Ninaongea na wewe unaendelea kula, ni mara ngapi umekula leo? Hii ni sahani yako ya 7 sasa, kula mchele,” MC aliuliza.

Ilionekana kuwa MC alikasirishwa na mgeni wa harusi kwa kuagiza vyakula vitamu vingi vilivyopikwa kwenye hafla hiyo, na kuzua hisia miongoni mwa watumiaji wa mitandao ya kijamii.

Katika video hiyo, anaonekana akiwaburudisha waliohudhuria katika mapokezi hayo.

 Tukio hilo lilikuwa la furaha huku umati wa watu wakifurahia chakula, muziki na sherehe.

Hali hiyo ilichukua hatua ya ucheshi wakati MC alipomwonyesha mgeni huyo, akiwa amevalia mavazi yake ya kitamaduni na kumtaka kueleza kwa nini anaagiza vyakula vya kipekee kwenye karamu.

View Comments