In Summary

•Msanii huyo mwenye ushawishi mkubwa alibainisha hafikirii kama anaweza kustahimili katika ulimwengu wa kisiasa.

•"Siasa sio kikombe changu cha chai na sijui wanasiasa wengi pia," alisema.

Akothee
Image: HISANI

Msanii na mjasiriamali Esther Akoth almaarufu Akothee amefichua wazi kuwa hana mpango wa kujiunga na siasa hivi karibuni.

Katika mahojiano ya hivi majuzi na gazeti la The Nairobi, mwanamuziki huyo mwenye ushawishi mkubwa alibainisha kwamba hafikirii kama anaweza kustahimili katika ulimwengu wa kisiasa.

Pia alisema kuwa hajui wanasiasa wengi licha ya kwamba yeye hukutana na baadhi yao katika maeneo ya umma ama wakati wa hafla kubwa.

"Mimi ni mwenye huruma na ninasema kama ilivyo. Sidhani kama naweza kustahimili katika siasa na sipendi uongo,” Akothee alisema.

Aliongeza, "Siasa sio kikombe changu cha chai na sijui wanasiasa wengi pia. Wakati mwingine nakutana nao kwenye  na wanapata hisia kwa sababu siwafahamu. Sitazami TV pia."

Akothee ni mmoja wa wasanii wanaofuatiliwa zaidi nchini Kenya na wenye ushawishi mkubwa nchini. Ana idadi kubwa ya watu wanaofuatilia maisha yake, na mara nyingi ameonekana akitangamana na wanasiasa wakuu na wenzi wao.

Takriban miezi miwili iliyopita, mwimbaji huyo alisherehekea mambo makubwa aliyofanikisha kufanya katika miaka yake ya 30.

Katika taarifa kwenye ukurasa wake wa Instagram, mama huyo wa watoto watano alifichua kuwa akiwa na umri wa miaka 31, tayari alikuwa amejijengea nyumba, akajengea wazazi wake na nyanyake.

Pia alibainisha kuwa wakati huo tayari alikuwa akiwalea watoto wake peke yake, akiendesha biashara na kufanya safari za kimataifa.

“Nilikuwa na miaka 31, tayari nilikuwa nimejenga nyumba yangu ya kustaafu, nimewajengea wazazi wangu nyumba mpya kabisa nikawanunulia magari mawili mapya kabisa, nikamjengea bibi yangu nyumba,” Akothee aliandika chini ya picha ya nyumba yake, nyumba ya mzazi wake na ile ya nyanya yake.

Aliongeza, “Mbali na kulea watoto wangu peke yangu, nilikuwa nikiwasaidia ndugu zangu, nikiendesha biashara zangu, nikihama kutoka mahakama moja hadi nyingine nikipigana vita vya baba za watoto wangu, kusafiri kwa ndege katika eneo la biashara, ndege za kibinafsi na mengine, kujenga taaluma yangu, kutafuta elimu yangu, na kungaa na kuishi kwa usawa.”

Msanii huyo mwenye umri wa miaka 43 alibainisha kuwa sasa amepata mengi na amepata usawa wa maisha na amani.

“Sasa nimepata usawa na amani. Nilifanya yote niliyotaka kufanya katika miaka yangu ya 30 sasa ninafurahia maisha yangu katika miaka yangu ya 40 na kusawazisha cheki zangu & kujitunza wazazi wangu na biashara zangu, kurudisha kwa jamii na kujenga urithi💪," alisema.

Aliongeza, “Sasa ninapata mapenzi, kuachwa na kuachana pia na  tunasonga mbele 🤣🤣🤣 shoneni vitenge bibi harusi bado yuko fiti."

Akothee pia alibainisha kuwa watoto wake wote wanafanya kazi na wako thabiti, jambo ambalo anajivunia sana.

View Comments