04 November 2015 1 Min Read
COTU yataka wanachama wake kuongezwa mishahara
by Brian Ndungu Habari
Picha: kahawatungu.com
Muungano wa vyama vya wafanyikazi COTU umewataka wanachama wa  vyama vyake tanzu kuitisha nyongeza ya mishahara na marupurupu kutoka kwa waajiri, ili kuwawezesha kumudu hali ngumu ya uchumi.
Katibu mkuu wa COTU Francis Atwoli amesema malipo ya sasa hayawezi kustahimili ongezeko la bei za bidhaa na gharama za huduma kama vile usafiri na kodi za nyumba.