11 June 2019 1 Min Read
Botswana yafutilia mbali sheria inayoharamisha mapenzi ya Jinsia moja
by Yusuf Juma Habari
Nchi ya Botswana imefutilia mbali sheria ya enzi za ukoloni iliyoharamisha mapenzi ya jinsia moja katika kesi kubwa iliyokuwa ikifuatiliwa na watu wengi barani afrika .
Uamuzi huo wa Botswana unajiri siku chache tu baada ya Kenya hivi maajuzi kutilia mkazo msimamo wa kuharamisha mapenzi ya jinsia moja .
Mahakama kuu jijini Gaborone imesema sheria iliyokuwa ikitoa adhabu kali kwa ushoga na mapenzi ya jinsia moja wa jumla ilikuwa kinyume na katiba .