Jackie Maribe

Urafiki wa kufaana . Ndio  taswira inayoweza kueleza uhusiano kati ya mwanahabari Jacque Maribe na Mkurugenzi wa mawasiliano ya kidijitali  katika Ikulu ,Dennis Itumbi . Maribe  siku ya jumatano ‘alirudisha mkono’ kwa kumtembelea Itumbi  katika makao makuu ta DCI wakati alipokamatwa kuhusiana na barua yenye madai ya kuwepo njama ya kumuua naibu wa rais William Ruto.

Itumbi  amekuwa akihudhuria vikao vya kesi ya mauaji inayomkumba Maribe  na mpenziwe wake  wa  zamani Joseph Irungu ,na masaibu yaliomfika  ,jumatano yalitoa  fursa  kwa mwanahabari huyo kwenda kumwona .

Maribe na Jowie wanakabiliwa na kesi ya mauaji ya mfanyibiashara Monica Kimani katika nyumba za  Lamuria Gardens mwaka wa 2018 . Maribe na Itumbi  wana historia ndefu lakini iliyoghubika usiri kuhusu hali ya uhusiano wao  sasa kwani kwa wakati mmoja  walidaiwa  kuwa wapenzi .

View Comments