10 August 2019 1 Min Read
Mkasa:Zaidi ya watu 50 wafariki katika mlipuko wa trela la mafuta Morogoro
by Yusuf Juma Habari
Takriban watu 57 wameafariki katika mlipuko wa trela la kubeba mafta nchini Tanzania ,polisi wamesema . Picha zilizowekwa mtandaoni zinaonyesha moto mkubwa ukiteleteza sehemu kubwa ya eneo huku miili yenye majeraha ya moto ikitapakaa kote .
Ripoti ambazo hazina ithibati zinasema kwamba atu walikuwa wakijaribu kufyonza mafuta kutoka kwa gari hilo ambali lilibingiria wakati mlipuko ulipotokea . Kisa hicho kimefanyika Morogoro yapata kilomita 200 magharibi mwa Jiji la Dar es salaam .
Mji wa morogoro ni kitovu muhimu cha usafirishaji wa mafuta kutoka bandari ya Dar .Kuna hofu kwamba idadi ya walioangamia huenda ikaongezeka .