Mkasa:Zaidi ya watu 50 wafariki katika mlipuko wa trela la mafuta Morogoro

Eneo la mkasa wa mlipuko wa trela la mafuta Morogoro ,Tanzania
Eneo la mkasa wa mlipuko wa trela la mafuta Morogoro ,Tanzania
Takriban watu 57 wameafariki  katika mlipuko wa trela la kubeba mafta nchini  Tanzania ,polisi wamesema . Picha zilizowekwa mtandaoni  zinaonyesha moto mkubwa ukiteleteza sehemu  kubwa ya eneo huku miili yenye majeraha ya moto ikitapakaa kote .

Ripoti ambazo hazina  ithibati zinasema kwamba  atu walikuwa wakijaribu kufyonza mafuta  kutoka kwa gari hilo ambali lilibingiria wakati  mlipuko ulipotokea . Kisa hicho  kimefanyika Morogoro yapata kilomita 200 magharibi mwa Jiji la Dar es salaam .

Mji wa morogoro ni kitovu muhimu cha usafirishaji wa mafuta  kutoka bandari ya Dar .Kuna hofu kwamba idadi ya walioangamia huenda ikaongezeka .