Daah! Waume wa kanisani pia? Mwanamke auawa na mumewe
Inasemekana kuwa Jamaa mmoja kutoka nchi ya Ghana na mhudumu katika kanisa la Assembly of God, alimuua mke wake mwenyewe.
Mwanamke ambaye alijitambulisha kama Bi Shirley Tackie, jirani alisema kuwa marehemu Dorcas na mume wake Prince Korley walikuwa na maisha mazuri sana bila mvurugano wala vita.
Zaidi ya hayo, binti huyu alisema kuwa kutokana na vile ambavyo anamjua Bwana Commodore hakuna mtu ambaye angeweza kufikiri kuwa bwana huyu anaweza kufanya kitendo kama kilecha kinyama.
''Tumewaona wawili hawa wakienda kanisani kila jumapili na kurudi nyumbani na furaha kila wakati.'' Shirley alisema.
Vilevile, mwanamke huyu alisema kuwa wawili hawa walikuwa wanahudhuria sherehe zozote au mikutano yoyote kanisani pamoja kila mara.
Ni dhahiri kuwa, wengi hawaamini kitendo hiki kwani si kawaida kwa binadamu haswa wanaomjua mungu kufanya kitendo kama hiki.
Mungu ailaze roho ya Bi Dorcas Anafi mahali pema peponi.