collabo
Mwaka wa 2019 umekuwa wa kufana sana katika sekta ya sanaa nchini kwani kando na miaka iliyopita, wasanii wetu wamejikakamua kisabuni. Kutoka wasanii waliokithiri, kina Khaligraph, Sauti Sol, Nameless, Wahu hadi wasanii wa kizazi kipya kina; Ethic, Ochungulo family na Sailors wote wameonesha ubabe wao kupitia nyimbo walizozindua.
Isitoshe, baadhi yao wameonesha uhodari wao na kuvuka mipaka ambapo wameweza kufanya collabo na wasanii kutoka mataifa jirani, huku Tanzania ikiwa kivutia kikuu cha wasanii hawa.
Radio Jambo hii leo tunakupa orodha ya collabo kumi bora zilizofanywa na wasanii kutoka Kenya na Bongo mwaka huu.
1. Nandy ft Sauti Sol - Kiza Kinene
Kusema wimbo huu ulizinduliwa wiki moja tu iliyopita na kulingana nami, tayari huu ni wimbo wa mwezi! Nandy amewashirikisha magwiji hawa wa Afrika na kuonesha upande tofauti sana, kwani watu wamezoa nyimbo zao huwa za party ama zimejaa vidosho wenye makalio kweli.
Wimbo huu tayari umetazamwa zaidi ya mara milioni moja, Youtube.