16 January 2020 1 Min Read
BREAKING NEWS: MKASA: Watu 5 wa familia moja wafariki Mwatate
by Yusuf Juma Habari
Watu watano wamefariki katika eneo la Kighombo huko Mwatate mkaunti ya Taita Taveta baada ya maporomoko ya ardhi kuivunika nyumba yao kufuatia mvua kubwa inayonyesha katika eneo hilo . Waliofariki ni Mwanamme mmoja ,mkewe na watoto wao watatu . Miili ya mwanamme huyo,mkewe na mtoto mmoja imepatikana huku juhudi za kuitafuta miili miwili ya watoto wao wengine ikiendelea .
Kamishna wa kaunti hiyo Rhoda Onyancha amewatahadharisha wakaazi wa Voi na sehemu nyingine zilizo katika hatari ya kukumbwa na maporomoko ya ardhi kuhamia maeneo yenye miinuko yaliyo salama .