05 February 2020 1 Min Read
TUNZA MTOTO WAKO!Kizaaza katika boma la Kutuny baada ya mwanamke kudai fedha za matumizi ya mtoto waliyezaa naye
by Yusuf Juma Habari
Kulikuwa na patashika katika boma la mbunge wa cherangany Joshua Kutuny mtaani Hardy wakati mwanamke mmoja alipowasili huko akidai kwamba mbunge huyo amemtelekeza mtoto waliyezaa naye .
Joyline Chemutai anadai kwamba mbunge huyo hajakuw aakituma pesa za kumsaidia mwanawe . Polisi wamesema walipewa taarifa kuhusu kizaazaa katika boma la mbunge huyo mwezi wa saa sita usiku .
Polisi waliojibu tukio hilo walielekea kwa Kutuny na kumpata mwanamke huyo akipiga kelele . katika patashika hiyo afisa mmoja wa polisi kwa jina Emmanuel Maiyo alifyatua risasi hewani ili kuleta utulivu .