Back with A bang!Marya Prude ajitokeza baada ya kutengana na Willis Raburu
Mamepa mwezi mei palizuka habariu za kutengana kwa Marya Prude na mumewe Willis Raburu na hata kipusa huyo akalazimika kuondoka nyumba waliokuwa wakiishi pamoja katika barabara ya Kiambu .
Habari za kutengana kwao zilisambaa mitandaoni kama moto katika kichaka kikavu na kwa sababu Marya ni mtu anayependa usiri wake alilazimika kujiondoa kwa muda kutoka mitandao ya kijamii . . Lakini kutokana na hatua alizochukua wiki hii yaonekana ameanza kureja tena mitadaoni na hata labda kupona makovu yaliyotokana na kutengana kwao .
Hakuna kati yao aliyezungumza kuhusu kilichotokea lakini labda kuna jambo zuri kuwa na matumaini katika masuala ya mapenzi .
Willis Raburu na Marya Prude walifunga ndoa miaka mitatu iliyopita na wameyapitia mengi tangia hapo ikiwemo kumpoteza mtoto wao aliyekuwa amezaliwa .