Mamepa mwezi mei palizuka habariu za kutengana kwa Marya Prude na mumewe Willis Raburu na hata kipusa huyo akalazimika kuondoka nyumba waliokuwa wakiishi pamoja katika barabara ya Kiambu .
Habari za kutengana kwao zilisambaa mitandaoni kama moto katika kichaka kikavu na kwa sababu Marya ni mtu anayependa usiri wake alilazimika kujiondoa kwa muda kutoka mitandao ya kijamii . . Lakini kutokana na hatua alizochukua wiki hii yaonekana ameanza kureja tena mitadaoni na hata labda kupona makovu yaliyotokana na kutengana kwao .
Hakuna kati yao aliyezungumza kuhusu kilichotokea lakini labda kuna jambo zuri kuwa na matumaini katika masuala ya mapenzi .
Willis Raburu na Marya Prude walifunga ndoa miaka mitatu iliyopita na wameyapitia mengi tangia hapo ikiwemo kumpoteza mtoto wao aliyekuwa amezaliwa .