Rais mstaafu Mwai Kibaki hayupo hospitalini .katibu wake wa kibinafsi  Ngari Gituku  amesema ingawaje ni kweli kwamba kibaki alikuwa hospitali maajuzi ,ilikuwa ni uangalizi wa kawaida na hajalazwa .

Gituku ametaja kama  ‘kuongezwa chumvi’ kwa ripoti katika vyombo vya habari kwamba Kibaki amekuwa hospitalini kwa siku kumi . Amesema Kibaki alitibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani .

Msaidizi huyo wa Kibaki amesema   hapafai kuwa na  hofu wakatu mtu mashuhuri anapopelekwa hospitalini  kwani ni jambo la kawaida kufanyiwa uangalizi wa kila mara .

Kibaki amekuwa na tatizo la goti tangu alipohusika katika ajali ya barabarani mwaka wa 2002  huo Machakos akifanya kampeini . Amekuwa akifanyia uangalizi na matibabu ya goti hilo tangia wakati huo .

View Comments