30 June 2020 1 Min Read
Kibaki hayupo Hospitalini –Msaidizi
by Yusuf Juma Habari
Rais mstaafu Mwai Kibaki hayupo hospitalini .katibu wake wa kibinafsi Ngari Gituku amesema ingawaje ni kweli kwamba kibaki alikuwa hospitali maajuzi ,ilikuwa ni uangalizi wa kawaida na hajalazwa .
Gituku ametaja kama ‘kuongezwa chumvi’ kwa ripoti katika vyombo vya habari kwamba Kibaki amekuwa hospitalini kwa siku kumi . Amesema Kibaki alitibiwa na kuruhusiwa kurejea nyumbani .
Msaidizi huyo wa Kibaki amesema hapafai kuwa na hofu wakatu mtu mashuhuri anapopelekwa hospitalini kwani ni jambo la kawaida kufanyiwa uangalizi wa kila mara .
Kibaki amekuwa na tatizo la goti tangu alipohusika katika ajali ya barabarani mwaka wa 2002 huo Machakos akifanya kampeini . Amekuwa akifanyia uangalizi na matibabu ya goti hilo tangia wakati huo .