03 July 2020 1 Min Read
Uhuru ahamia Jumba la Harambee kutoka Ikulu kwa ajili ya COVID 19
by Yusuf Juma Habari
Rais Uhuru Kenyatta amehamia jumba la Harambee baada ya ikulu kufungwa wafanyikazi wanne walipopatikana na virusi vya corona .
Rais Kenyata amesema hajapatikana na virusi hivyo na amekuwa akifanya kaz katika jumba la Harambee iliyotajwa kuwa salama .wafanyikazi wake pia wamehamia jengo hilo naye .
Rais Kenyatta amekuwa akifanyia kazi Ikulu ya Nairobi hadi visa vya corona vilivporipotiwa Juni tarehe 15 katika makao hayo yake .mikutano yake yote sasa imekuwa ikifanyika Harambee .
Kabla ya visa hivyo vya corona kuripotiwa Ikulu rais alikuwa akiandaa mikutano yake yote ikiwemo na wabunge na baadhi ya wanasiasa katika Ikulu .