Messi The great: Ashinda tuzo ya 7 ya golden Boot katika La Liga
Lionel Messi ameshinda tuzo yake ya saba ya mfungaji wa mabao mengi katika La liga na yake ya nne mfululizo baada ya kuifungia Barcelonamabao mawili katika ushindi wao wa 5-0 dhidi ya kilabu ya Alaves katika siku ya mwisho ya ligi hiyo ya uhispania .
Nahodha huyo wa Barcelona alimaliza kwa mabao 25 ,manne mbele ya mshambuliaji wa Real Madrid Karim Banzema . mchuano huo hata hivyo haukuwa muhimu wa Barca kwani tayari walikuwa wameshalinyakua taji hilo siku ya alhamisi .
Messi alifaulu kumkanganya mlinda lango ili kufunga mabao mawili huku Ansu Fati, Luis Suarez na Nelson Semedo wakifunga mabao mengine .
Riqui Puig, Messi na Arturo Vidal wote waligonga mkuti kabla ya Fati kufungua mwanzo wa mabao .
Hii ndio ya kwanza kwamfungaji bora wa La liga kufunga chini ya mabao 30 tangu nyakati za Daniel Guiza wa Mallorca miaka 12 iliyopita .