Kalonzo atamatisha mkataba na Nasa ,ajiunga rasmi na Jubilee
Kiongozi wa chama cha Wiper Kalonzo Musyoka ametnagaza mipango ya kujiondoa rasmi kutoka muungano wa NASA unaoongozwa na Raila Odinga ili kujiunga na Jubilee .
Kamati ya usimamizi wa chama cha Wiper ilikutana kupitia njia ya mtandao na kupitisha uamuzi wa kujiunga katika muungano na chama cha Jubilee kinachoongzowa na rais Uhuru Kenyatta .
Hatua hiyo sasa inamaanisha kwamba iper sasa itaondoka kutoka muungano huo wa upinzani kwani sheria hairuhusu chama kimoja kuwa katika zaidi ya muungan mmoja .
Chama cha Kalonzo pia kitalazimika kumuandikia msajili wa vyama Anne Nderitu kumfahamisha rasmi kuhusu uamuzi wa kujiondoa kutoka NASA na kuiunga na muungano mpya .
Ili muungano wa NASA kuvunjiliwa mbali kabisa vyama tanzu vitatu vinafaa kuondoka lakini kwa sasa ODM ,ANC na Ford Kenya bado vipo katika muungano huo .